June 16, 2022
June 16, 2022
Viwanja vya Furahisha
SIKU YA MTOTO WA AFRIKA
Siku ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa kila Mwaka tarehe 16 Juni baada ya kupitishwa kwa Azimio la nchi 51 wanachama wa Umoja wa Nchi huru za Afrika (OAU). Tanzania kama nchi mwanachama wa Umoja wa Umoja wa Afrika imekuwa ikiadhimisha siku hii tangu mwaka 1991. Lengo la kuadhimisha siku hii ni kukumbuka mauaji ya kinyama waliyofanyiwa watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini mwaka 1976.
Katika ngazi ya Mkoa wa Mwanza Maadhimisho haya yatafanyika katika Viwanja vya Furahisha na Mgeni Rasmi Atakuwa mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi. Robert Gabriel Luhumbi, na Muda ni kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 12 jioni.
USHIRIKI WA BEYOND GIVING
Kama mdau wa Maendeleo Tutashiriki, kwa kufanya Tathimini na Mazoezi kwa watoto wenye ulemavu
Share This Event