Siku ya Kimataifa ya Watu Wenye Ulemavu, au Siku ya Walemavu Duniani, huadhimishwa kila mwaka tarehe 3 Disemba. Inalenga kuongeza ufahamu wa mateso ya watu wenye ulemavu katika nyanja zote za kitamaduni, kijamii, na kisiasa huku ikikuza haki na ustawi wao katika viwango vyote vya jamii na maendeleo.
Siku ya Kimataifa ya Wanawake, kampeni ya kila mwaka ya Umoja wa Mataifa ya kuhamasisha juhudi za kuleta usawa wa kijinsia duniani kote, mwaka huu inaadhimishwa kesho Ijumaa, kaulimbiu ikiwa ni "Wekeza kwa wanawake: Ongeza kasi ya maendeleo ."
Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) kwa kushirikiana na mashirika wadau wa elimu na Serikali, wanafanya maadhimisho ya Juma la elimu mkoani Morogoro, ambapo asasi za kiraia zimekumbushwa wajibu wa kuchangia juhudi za Serikali katika kuboresha elimu.
Siku ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa kila Mwaka tarehe 16 Juni baada ya kupitishwa kwa Azimio la nchi 51 wanachama wa Umoja wa Nchi huru za Afrika (OAU). Tanzania kama nchi mwanachama wa Umoja wa Umoja wa Afrika imekuwa ikiadhimisha siku hii tangu mwaka 1991.
Hivi sasa SIKU YA HEDHI SALAMA DUNIANI haiadhimishwi na waanzilishi pekee (WASH United), lakini pia mashirika na wanaharakati mbalimbali wanaoguswa na suala hili. BEYOND GIVING pia itashiriki kama Mdau na Muhamasishaji katika maswala ya hedhi na hasa kwa watoto wa kike wenye ulemavu.